PATA GARI LA BURE

PATA GARI LA BURE
bonyeza neno APPLY kwenye picha juu ujishindie gari

Aug 1, 2015

Azam FC imetinga hatua ya fainali za CECAFA Kagame Cup kwa mara ya pili baada ya kuichapa KCCA ya Uganda bao 1 - 0 na sasa itacheza fainali jumapili usiku katika dimba la uwanja wa taifa na Gor Mahia ya Keny.
Sifa zimwendee winga Farid Mussa aliyepachika bao hilo dakika ya 76 baada ya kupokea krosi nzuri ya Ame Ally. Katika mchezo huo ambao kwa mara nyingine beki , Muivory Coast Serge Wawa kachaguliwa kuwa mchezaji bora 'Man of the Match.
Azam FC ilikuwa ishangilie ushindi huo mapema kupitia kwa straika Muivory Coast Kipre Tchetche katika dakika ya 33 na 39 lakini ya mashuti yake kutoka nje.
Hata hivyo, mlinda lango, Aishi Manula alifanya kazi ya ziada dakika ya 36 alipookoa shuti la Sserunkuma Isaac ikawa kona tasa.
Azam FC ililiandama lango la KCCA baada ya kocha Stewart Hall kufanya mabadiliko kipindi cha pili kwa kuwatoa Mudathir Yahya na naasi yake kuchukuliwa na Ame Ally, Erasto Nyoni akaingia Shomari Kapombe na Kipre Tchetche akaingia Didier Kavumbagu.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Erasto Nyoni/ Shomari Kapombe, Said Morrad, Aggrey Morris, Wawa, Mugiraneza, Mudathir Yahya/ Ame Ally, Domayo, Tchetche/ Kavumbagu, arid Mussa, John Bocco,

No comments:

Post a Comment