PATA GARI LA BURE

PATA GARI LA BURE
bonyeza neno APPLY kwenye picha juu ujishindie gari

Aug 8, 2015

YANGA KULIPIZA KISASI KWA AZAM

Mabingwa wa Kombe la Afrika Mashariki “Kagame Cup”, Azam FC inatarajia kuanza mazoezi leo Ijumaa asubuhi ikielekea Kisiwani Zanzibar kwa ajili ya maandalizi zaidi.

Azam FC inaingia msituni kujiwinda na mechi yao ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga itakayochezwa mwishoni mwezi huu kabla ya kuanza kwa mikikimikiki ya Ligi Kuu Bara.

Kocha mkuu wa kikosi hicho, Stewart Hall aliwapa mapumziko wachezaji wake mara tu baada ya kuchukua ubingwa huo uliowafanya waandike historia mpya kwani ni mara ya kwanza kutwaa Kombe hilo pia walicheza bila kuruhusu bao hata moja langoni mwao.

Kocha msaidizi wa Azam FC, Dennis Kitambi alisema: "Tunatarajia kuanza mazoezi Ijumaa na baada ya hapo, tutaelekea Kisiwani Zanzibar kwa ajili ya maandalizi zaidi ya mechi yetu ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga."

"Sijajua ni siku kamili ya safari lakini inaweza kuwa Ijumaa hiyo hiyo jioni baada ya mazoezi au siku ya Jumamosi,"alisema Kitambi wakati wa halfla ya kumkabidhi Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Kikwete kikombe.

Azam itacheza na Yanga mechi hiyo baada ya kumaliza nafasi ya pili kwenye ligi na Yanga ikiwa ni mabingwa.

No comments:

Post a Comment